TANGAZA NASI

header ads

Chadema jimbo la Makambako wazindua kampeni,watoa wito kuchagua viogozi wenye uwezo

 



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Njombe kimewataka wanachama wa chama hicho na wananchi kwa ujumla kuchagua viongozi wenye uwezo wa kutatua changamoto zinazowakabili katika maeneo yao.

Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Njombe Rose Mayemba wakati wa uzinduzi wa kampeni za mgombea wa ubunge  jimbo la Makambako,ambapo amewataka wanachama na wananchi kwa ujumla kumchagua mgombea wa nafasi ya ubunge kupitia chama hicho kwa kuwa ana uwezo wa kuwasilisha na kutatua changamoto zao.

Aidha mwenyekiti amesema chama chake kimejipanga kushinda katika uchaguzi huo kuanzia ngazi ya Urais,Ubunge na Udiwani katika maeneo yote ambayo wamesimamisha wagombea.

“Tuleteeni mtu ambaye akienda kupaza sauti kule huku utakuta maji yanatanda,na mchagueni General Kaduma kwasababu ana ajenda za Makambako na ajenda za kitaifa”alisema Rose Mayemba

Naye mgombea wa ubunge jimbo la Makambako General Reuben Kaduma amesema endapo atapata ridhaa kwa wananchi na kuwa mbunge atahakikisha anawasaidia wananchi katika kutatua changamoto zinazowakabili katika sekta ya kilimo,afya,maji na elimu.

“Dhamira nikuwaletea heshima na maendeleo Makambako,watu wanahusika kwenye biashara,kilimo lakini manufaa ni madogo,nimeona niweze kuwatumikia wanamakambako ili tuweze kusonga mbele”alisema General Reuben Kaduma

Hata hivyo baadhi ya wagombea wa udiwani kupiti chama hicho Akiwemo mgombea udiwani kata ya Makambako Daud Tweve,Mgombea udiwani kata ya kivavi, Baraka  Kivambe,mgombe udiwani kata ya mwembetogwa Sillas Makweta na mgombea udiwani kata ya kitisi Seth Vegulla wamewaomba wananchi kuwapatia kura zao kwa kuwa wana agenda za kimaendeleo katika kata hizo.

Tayari tume ya Taifa ya uchaguzi NEC ilishatangaza kuanza kampeni kuanzia Agosti 26 mwaka huu na vyama vya siasa vinaendelea na kampeni hizo kwa ajili ya kuendelea na uchaguzi mkuu wa Oktoba 28 mwaka huu.

 

Post a Comment

0 Comments