TANGAZA NASI

header ads

Wagombea wa vyama vinne Jimbo la Makete wapitishwa na NEC

 

 


Na Henrick Idawa,Makete

Wagombea wote wa Ubunge jimbo la Makete Mkoani Njombe wametangazwa kuwa ni wagombea halali na hata mmoja wao hajawekewa pingamizi baada ya muda wa mapingamizi kumalizika huku mapingamizi yakijitokeza kwa upande wa madiwani katika kata mbalimbali

Akizungumza na kituo hiki ofisini kwake Msimamizi msaidizi wa uchaguzi jimbo la Makete Fadhili Nkenza amesema wagombea hao wa ubunge kutoka vyama vinne wanatakiwa kuendelea na hatua zinazofuata kwa kuwa hawajawekewa pingamizi

“Hatujapokea pingamizi hata moja hivyo wagombea wote w vyama vinne,Festo Richard Sanga wa CCM,Joma Mwakisitu wa ACT wazalendo na Ahady Tweve wa Chadema pamoja na Grace Njekela wa NCCR Mageuzi wote ni wagombea halali wa nafasi za ubunge kwa hiyo wataruhusiwa na kampeni kwa mujibu wa ratiba zetu” Fadhili Nkenza Msimamizi  msaidizi wa Uchaguzi jimbo la Makete

 Kwa upande wa udiwani Msimamizi huyo wa uchaguzi amezitaja kata ambazo wagombea wamewekewa pingamizi na wanatarajia kutoa uamuzi wa mapingamizi hayo kesho Agosti 27,2020

“Kuna pingamizi kutoka kata ya Lupila ambapo mgombea wa chama cha Mapinduzi amempinga mgombea wa Chadema,kuna pingamizi pia kata Mbalanze hawa wote wamepingana wa Chadema amepinga wa CCM na wa CCM amempinga wa Chadema,Kata ya Iwawa mgombea wa CCM amempinga wa Chadema,kata ya Kipagalo wote walipingana na kata ya Luhumbu pia vyama vitatu vya ACT,NCCR na CCM walipingana,Kata ya Lupalilo CCM walimpinga mgombea wa Chadema lakini pia na kata zingine waliendelea kupingana”aliongeza Fadhili Nkenza Msimamizi  msaidizi wa Uchaguzi jimbo la Makete

 

 

 

Post a Comment

0 Comments