TANGAZA NASI

header ads

Israel yashusha shambulizi la tatu mfululizo Gaza

 

Ndege za kivita za Israeli zimeishambulia Gaza kwa mara ya tatu mfululizo tangu jana jioni.

Msemaji wa jeshi la Israeli Avichay Adraee amesema kwenye akaunti yake ya Twitter kwamba ndege za kivita za Israeli zimeshambulia vifaru vya Hamas kusini mwa Gaza.

Adraee amebaini kuwa shambulizi hilo limetekelezwa dhidi ya makombora 7 yaliyorushwa kutoka Gaza, 6 kati ya makombora hayo yaliangamizwa na mfumo wa ulinzi wa nchi hiyo.

Katika taarifa za awali kwenye vyombo vya habari vya Israeli na mitandao ya kijamii, ilibainika kuwa kombora lililorushwa kutoka Gaza liligonga nyumba moja katika mji wa Sderot.

Licha ya shambulizi hilo, Israel imekuwa ikiishambulia Gaza tangu jana jioni.

Post a Comment

0 Comments