TANGAZA NASI

header ads

“Rais amenipa kibali nikashughulike na maswala mengine ya kisiasa”Aliye kuwa DC Wanging’ombe Ally Kasinge aaga




Na Amiri Kilagalila,Njombe

Aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Wanging’ombe Ally Kasinge ameishukuru serikali na Chama cha Mapinduzi kupitia Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumuamini na kumpa nafasi ya uongozi kama mkuu wa wilaya hiyo kwa miaka minne mpaka hapo jana July 7 nafasi yake ilipochukuliwa na kiongozi mwingine.

Kasinge ametoa shukrani zake kupitia vyombo vya habari wakati akiwaaga wananchi wa wilaya ya Wanging’ombe na viongozi wote wa Chama na Serikali.

“Namshukuru sana Mh,Rais alipoendelea kuniamini na kuniteua kuwa mkuu wa wilaya ya Wanging’ombe tangu tarehe 26  mwezi wa 6 mwaka 2016 kwa hiyo nimeweza kutumika kwa miaka minn na siku kama 11,kwa hiyo nina kila sababu ya kumshukuru Mh,Rais kwa kuniamini na kubaki katika nafasi kwa kipindi chote hicho,lakini pili ninamshukuru kwa kuendelea kuniamini kubaki kwa kipindi hicho chote mpaka pale ambapo amenipa kibali kwa kile ambacho nimeomba ili nikashughulike na maswala mengine ya kisiasa”alisema Kasinge

Aidha amekishukuru Chama cha Mapinduzi

“Nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipokishukuru Chama change cha Mpainduzi,ndicho ambacho kimenilea katika tasnia ya uongozi na maadili ya uongozi,uzalendo,utiifu ,uchapa kazi na uwajibikaji.kwa kweli nakishukuru sana Chama cha mapinduzi ndicho ambacho kimenifikisha hapa,na nitaendelea kuwa mwaminifu katika Chama changu cha Mapinduzi na kuendelea kuwa mwaminifu katika nchi ya ngu”

Aishukuru serikali ya mkoa wa Njombe

“Niishukuru sana serikali ya mkoa wa  Njombe ambapo nimetumika wakuu wa mikoa wawili na nimekuwa na Mh,Christopher Ole Sendeka Kaka yangu tumefanya naye kazi vizuri sana na alinilea katika maadili ya kazi,uzalendo na utiifu katika nchi,kwa kweli ni kiongozi wa namna yake wa kuigwa”alisema Kasinge

Hata hivyo Kasinge amewashukuru wananchi wa 
Wanging’ombe,watumishi  serikali na Chama kwa kuwa malengo waliyokusudia ya kuyafanya kwa kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi yamekamilika kwa asilimi 90 mpaka 100.

Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli jana Julai 07,2020 alifanya uteuzi wa Mkuu wa wilaya mmoja na wakurugenzi wa Halmashauri watano katika mikoa mbalimbali. 

Rais Magufuli alimteua Lauteri Kanoni kuwa Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Mkoani Njombe akichukua nafasi ya Ally Kasinge,ambapo kabla ya uteuzi huo Kanoni alikuwa Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Serikali za Mitaa huko Mkoani Songwe.




Post a Comment

0 Comments