TANGAZA NASI

header ads

Wasaidizi wa kisheria nchini watakiwa kuzingatia maadili




Na Amiri Kilagalila,Njombe

Wasaidizi wa kisheria nchini wameelezwa kuzingatia maadili katika utoaji wa huduma za msaada wa kisheria kwa wahitaji ili waweze kupata nafuu na haki inayohitajika kwa mujibu wa sheri.

Wito umetolewa na katibu mkuu wa wizara ya katiba na sheria Prof.Sifuni Mchome wakati akizindua kamati ya uratibu wa shughuli za msaada wa kisheria mkoa wa Njombe.

“Katika kazi ni wajibu kuhakikisha maadili yanazingatiwa,maadili katika maeneo mbali mbali,maadili katika ushauri,kupeleka kesi mahakamani na maadili katika mahusiano yetu na watu ambao tunawahudumia,na mtoa msaada wa kisheria hawezia akawa mchonganishi”alisema  Prof.Sifuni Mchome

Aidha Mchome amesema lengo mojawapo la serikali kuwa na wasaidizi wa msaada wa kisheria  ni kusaidia katika utetuzi wa migogoro inayojitokeza katika jamii pamoja na kuhakikisha uwepo wa utawala bora.

Naye mkuu wa mkoa wa Njombe  Christopher Ole Sendeka ameiomba wizara ya katiba na sheria kuongeza nguvu katika kuzisimamia asasi zinazotoa elimu kutokana na uwepo wa asasai zinazofanya kazi isiyokuwa na afya kwa taifa.

“Kwa muda mrefu huko nyuma asasi hizi zingine zilikuwa zikifanya kazi ambazo hazina afya kwa ustawi wa nchi na wengine wamekuwa ni madalali wa kusimamia maslai ya nchi zingine za ughaibuni”alisema Ole Sendeka

Kaimu aifisa maendeleo ya jamii mkoa wa Njombe Farahani Kanyenda,amesema wasaidizi na watoa huduma za msaada  wa kisheria  wamekuwa na msaada mkubwa kwa jamii na kuwezesha idadi ya watu waliopata huduma ya msaada wa kisheria kwa kipindi cha Julai 2019 hadi Mei 20 kufika 8282 kwa upande wa madai,19 kwa upande wa Jinai,26 kwa upande wa matunzo huku watoto waliopata msaada wa kisheria wakiwa 42.

Erasto Mkiwa ni mratibu wa shirika la PAD na Geofrey Kaduma ni mkurugenzi wa kituo cha msaada wa sheria Njombe,wanasema licha ya uwepo wa changamoto katika shughuli zao lakini wanaamini kamati iliyoundwa itasaidia kuwafikia zaidi wananchi wenye migogoro mbali mbali.

“Kwa kupitia kamati hii itatusaidi kuwafikia zaidi wananchi kwasababu ni sehemu mojawapo ya kurahisisha mawasiliano na kupitia wadau tuliopo ni rahisi kuelewa wapi kuna tatizo”Alisema Erasto Mkiwa


Post a Comment

0 Comments