Na
Jackline Kuwanda, DODOMA.
Recho
Steven kutoka Shirika la Plan international amesema kuwa wamekuwa
wakishughulika na mradi wa usafi wa mazingira Tanzania lengo likiwa ni
kuhakikisha kuwa jamii zinabadili tabia katika masuala ya usafi wa mazingira
kwa ujumla wake kuanzia ujenzi wa vyoo bora ,matumzi ya vyoo bora,unawaji wa
mikono ,masuala ya hedhi salama kwa watoto wa kike pamoja na wanawake kwa
ujumla.
Akizungumza
Siku ya Hedhi Duniani iliyoadhimishwa May 28,Recho amezungumzia hali ya
mila,Tamaduni ambazo zimechangia suala la hedhi kutozungumziwa kwa wazi na
kusababisha watoto wa kike kukosa masomo kipindi ambacho wako katika hedhi.
Amesema
kuwa watoto wa kike wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali ikiwa ni
pamoja na kutokuwa na miundombinu rafiki ambayo wangeweza kujisitiri vyema
pindi wakiwa mashuleni .
Wakati
huo huo amesema kuwa mara nyingi watoto wanakosa masomo wakati wa hedhi ni wale
ambao wako katika shule za msingi .
kutokana
na hali hiyo pia amesema kuwa baadhi ya wazazi wanachangia kwa kiasi kikubwa
kwani wengine hufikia hatua ya kumuombea mtoto ruhusa kwa kisingizio kuwa
anaumwa.


0 Comments