Jeshi la Taifa la Somalia limefanikiwa kuangamiza wanachama saba wa kundi la kigaidi la al-Shabaab katika eneo la Hiran, katikati mwa nchi.
Kadhalika wanachama wengine kadhaa wa kundi hilo wamejeruhiwa katika operesheni hiyo ya jana Jumanne.
Operesheni hiyo imejiri siku moja baada ya jeshi la eneo lenye mamlaka ya ndani la Jubaland kutangaza habari ya kuangamiza wanachama wanne wa kundi hilo la kigaidi katika mji wa Dhobley, Kusini mwa Somalia.
0 Comments