TANGAZA NASI

header ads

Daktari wa Yanga akoshwa na uvaaji Barakoa wa Morrison




KITENDO cha nyota wa Klabu ya Yanga, Bernard Morrison kuvaa barakoa kwa muda wote aliokuwa kwenye mazoezi ya kikosi, kimemkuna daktari wa kikosi hicho, Shecky Mngazija ambaye hakusita kusifu usikivu wa nyota huyo raia wa Ghana.

Tofauti na wachezaji wengine waliofi ka mazoezini hapo ambao walivua barakoa zao wakati wa mazoezi lakini Morrison aliendelea kuivaa hadi alipoondoka uwanjani hapo.

Akizungumza na Championi Ijumaa, Mngazija alisema Morrison alionyesha mfano mzuri wa kuzingatia maagizo ambayo wachezaji walipewa ili kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona wanapokuwa mazoezini.

“Tuliwapa wachezaji wote utaratibu mzima wanaopaswa kuuzingatia ili kuendelea kuchukua tahadhari ya maambukizi ya Virusi vya Corona wanapokuwa kwenye mazoezi, kwa upande wangu kwenye mazoezi haya, Morrison ndiye aliyejitahidi kufuata utaratibu huo kwa asilimia nyingi zaidi kwa kuvaa barakoa yake muda wote wa mazoezi.

“Lakini pia nawapongeza wachezaji wengine ambao pia walionekana kufuata utaratibu kwa kunawa maji tiririka na sabuni na kuvaa barakoa zao wakati wanawasili, unajua huu ni utaratibu mpya kidogo kwao, hivyo wanahitaji muda kuuzoea nasi tunaendelea kuwasisitiza wachezaji wetu.

“Yanga iliyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara baada ya kujikusanyia pointi 51 katika michezo yake 27, jana iliendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Sheria uliopo Ubungo jijini Dar.

Stori; Joel Thomas,Dar es Salaam

Post a Comment

0 Comments