TANGAZA NASI

header ads

CAG Kichere aridhishwa na kasi ya ujenzi wa ofisi za ukaguzi Njombe



Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali nchini Bw,Charles E Kichere akizungumza na baadhi ya watumishi wa ofisi ya mkaguzi mkoa wa Njombe nje ya jingo jipya la ofisi ya mkaguzi linalojengwa Lunyanywi mjini Njombe.





Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali nchini Bw,Charles E Kichere akikagua moja ya chemba ya ofisi mpya za ukaguzi mkoa wa Njombe.







Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali nchini Bw,Charles E Kichere akikagua  ubora na kuta za jengo la ofisi mpya za ukaguzi mkoa wa Njombe.



Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali nchini Bw,Charles E Kichere,Akipata maelezo mafupi na mmpja wa ofisa ukaguzi mkoa wa Njombe juu ujenzi wa jengo hilo jipya la ofisi za ukaguzi.





Muonekano wa nje sehemu ya jengo la ofisi mpya za ukaguzi mkoa wa Njombe zinazojengwa Lunyanywi mkoani Njombe.






Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali nchini Bw,Charles E Kichere,Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ukaguzi wa jengo la ofisi za ukaguzi Njombe.




Na Amiri kilagalila,Njombe

Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali nchini Bw,Charles E Kichere,amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa ofisi ya Taifa ya ukaguzi mkoa wa Njombe inayoendelea kujengwa mkoani humo,huku akiagiza kukamilishwa kwa ofisi hizo kabla ya mwezi wa sita ili ziweze kutumika.

Akiwa katika eneo la jengo za ofisi hizo lililopo Lunyanywi halmashauri ya mji wa Njombe,Kichere amesema anahitaji majengo hayo kukamilika kabla ya mwezi wa sita ili watumishi wapate mazingira mazuri ya kufanya kazi.

“Majengo haya ni mazuri na yanaendelea vizuri nadhani itabidi mwaka huu kabla ya mwezi wa sita wamalizie kazi ndogo ndogo ambazo zimebaki ili tuingie kabla ya mwezi wa sita”alisema Kichere

Vile vile Kichere amesema ujenzi huo unaendelea katika mikoa mingine minne katika utekelezaji wa matakwa ya kuwa na ofisi binafsi mikoa yote ya Tanzania.

“Kwa hiyo tumekubalina na Serikali kwamba tuwe tunajenga ofisi kwa ajili ya sisi kuwa na ofisi zetu,sasa hivi tunaendelea kujenga ofisi mkoa wa Mara,Simiyu,Geita na hapa Njombe na ofisi zipo katika hatua mbali mbali za kuhamia”alisema Kichere

Katika hatua nyingine amesema ofisi ya Mkaguzi mkuu inategemea mwaka wa fedha 2020/2021 kuanza ujenzi wa ofisi katika mikoa mingine minne mara baada ya kukamilisha katika mikoa ambayo tayari ujenzi unaendelea.

“Lakini pia niishukuru Serikali tunapanga mwaka kesho kama mambo yatakuwa sawa tutaanza kujenga ofisi zetu katika mkoa wa Mwanza ambako tumepanga,mkoa wa Tanga,Katavi na mkoa wa Songwe ili kila mkoa tuwe na ofisi”aliongeza Kichere

Aidha Bw,Kichere amesema ujenzi wa ofisi za ukaguzi kila mkoa ni kutimiza matakwa ya viwango vya ukaguzi wa Kimataifa.

“Kwa sasa hivi tuna miradi ya kujenga ofisi za ukaguzi katika mikoa yetu yote ya Tanzania,ili kutimiza matakwa ya viwango vya ukaguzi wa kimataifa ambavyo vinataka sisi tuwe na ofisi ya kwetu badala ya kuwa tunakaribishwa tunakaa kwa wakaguliwa.Mfano ukienda Mara utakuta ofisi ya Mkaguzi iko ndani ya ofisi ya mkuu wa mkoa ambaye ni mkaguliwa wetu”alisema tena Kichere

Post a Comment

0 Comments