TANGAZA NASI

header ads

Waumini wajawa na furaha,kanisa mbioni kupata gari




Na Amiri Kilagalila,Njombe

Kanisa la Romani Katoliki parokia ya Utalingolo jimbo la Njombe mbioni kupata gari ya usafiri kwa ajili ya parokia kutokana na kukusanya Shilingi milioni hamsini na nne,laki tisa na arobaini na moja elfu,na mia nne hamsini (54,941,450/=) kutoka kwa wadau mbali mbali na harambee  iliyofanyika mapema August 2/2020 katika kanisa hilo.

Awali akitoa taarifa ya Parokia kwa niaba ya kamati ya harambee ya ukusanyaji wa fedha za ununuzi wa gari Ndug,Deo Mtewele amesema Parokia yenye vigango vinne vya Utalingolo,Igoma,Iliwa na Luhuji ilianzishwa rasmi mwaka 2011,lakini kumekuwa na shida ya utoaji wa huduma kutokana na kukosa usafiri huku ikilazimu kutumia njia mbali mbali ikiwemo kuazima kwa wadau

“Licha ya Changamoto ya usafiri lakini Parokia yetu imefanikiwa kufanya shughuli mbali mbali za kitume,pamoja na mafanikio moja ya changamoto yetu ni ukosefu wa gari ya Parokia kama chombo cha kurahisisha huduma mbali mbali za Kichungaji”alisema Deo Mtewele

Daktari Tobias Lingalangala ni mgeni wa heshima katika harambee ya ununuzi wa gari ilyofanyika katika kanisa hilo,kutokana na kuona changamoto za kanisa ameweza kuchangia shilingi Milioni 15 na kulitaka kanisa kutafuta gari mapema inayoweza kuendana na fedha iliyopatikana kuliko kusubiri kutafuta Milioni 100 ya makadilio na mahitaji yalio kuwa yamepangwa na kamati.

“Mtafute gari ambayo itakuwa nzuri na kwa hizi fedha mlizokusanya mkishirikiana na mimi kwa utulivu na kwa kuamini tunaweza kununua gari nzuri sana,kwa fedha hizi inawezekana” Alisema Dkt,Thobias Lingalangala Mgeni wa heshima harambee ya ununuzi wa gari ya Parokia ya Utalingolo,jimbo la Njombe.

Mwenyekiti wa kamati ya harambee Ndugu,Erasto Mpete amesema hawakuweza kutajia kupata kiasi hicho cha fedha kwa kuwa sio kitu kidogo kwao.

“Tukiongeza na kitita cha Mgeni rasmi kwenye fedha tulizokusanya jumla yake inatufanya kuwa na jumla ya milioni hamsini na nne laki tisa na arobaini na moja mia nne hamsini,kwa maneno mengine wanaparokia ya Utalingolo tumechanganyikiwa,kwa kweli tunamshukuru sana mgeni rasmi”alisema Erasto Mpete

Baadhi ya waumini wa kanisa hilo wamesema hatua waliyofikia ni jambo la kushukuru Mungu kwa kuwa wanaamini Parokia yao sasa kupata usafiri kwa ajili ya Paroko utakaomuwezesha kufika sehemu yoyote kwa wakati.

Post a Comment

0 Comments