TANGAZA NASI

header ads

Makete:Shule ya sekondari Lupila yapata,yawakaribisha kidato cha tano

 

Na Amiri Kilagalila,Njombe

 Wanafunzi wa Kidato cha tano katika shule ya sekondari Lupila iliyopo wilayani Makete mkoani Njombe,wametakiwa kufuata na kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa katika shule hiyo ikwemo kuepuka migomo ili waweze kufanikiwa kupata elimu bora itakayowasaidia katika maisha yao.

 Hayo yamebainishwa mwishoni mwa wiki katika sherehe za kuwakaribisha wanafunzi hao wa kidato cha 5 katika shule hiyo ambapo mgeni rasmi Kaimu Mtendaji wa kata ya Lupila Esau Pagalo amesema wanafunzi hao wanatakiwa kuzingatia masomo na wajiepushe na migomo.

 “Muwe tayari kusoma katika shule yetu hii ya Lupila,mnapofika hapa fateni na kuzingatia taratibu na sheria zilizowekwa hapa shuleni,walimu wapo tayari kuwa na ninyi na hatutegemei kabisa kutokea migomo”alisema Esau Pagalo

 Mkuu wa shule hiyo Mwl Abokasa Ngwale amesema walimu wa shule hiyo wamejipanga kuwafundisha ipasavyo wanafunzi hao huku  serikali ikiwa imewapangia wanafunzi 75 kwa maana kila mkondo wanafunzi 25, ambapo mpaka sasa wameripoti wanafunzi 50

 “Serikali ilitupangia wanafunzi 75 kwa EGM wanafunzi 25,HGK wanafunzi 25 na HKL wanafunzi 25 na kufanya jumla jumla 75 ingawa kama shule tuliomba wanafunzi 40 sasa tumeongezewa na hiyo sio changamoto kwetu” alisema Abokasa Ngwale

 Naye Mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi shuleni hapo Bw. Nuhu Sanga amesema michango ya wananchi inawasaidia kuendelea na ukarabati wa vyumba viwili vya madarasa ambavyo Wanatarajia kuvitumia kama mabweni

 “Hali ya ujenzi wa maeneo ya shule yanaenda vizuri japo sio sana kwasababu kuna mambo mengine bado hatujakamilisha,tunategemea michango kutoka kwa wananchi ili tuendelee kukarabati vyumba viwili vya kulala wanafunzi “alisema Nuhu Sanga

 Shule ya sekondari Lupila wilayani Makete mkoani Njombe  ni miongoni mwa shule zilizopewa kibali na kuanzisha kidato cha tano na sita mwaka huu 2020.

 

 

Post a Comment

0 Comments