Serikali ya Tanzania imenunua jiwe la kilo 6.3 la madini ya Tanzanite kutoka kwa mchimbaji Saniniu Laizer kwa shilingi za Tanzania bilioni 4.8.
"Jiwe hili jipya alilipata wakati wakiondoa miamba kwenye eneo ambalo walipata mawe mengine...walikuwa wakisafisha eneo kabla ya kuanza kuchimba upya," ameeleza Dotto Biteko, Waziri wa Madini Tanzania.
Kwa upande wake mchimbaji Laizer amewataka wachimbaji wengine kuwa wazalendo na kuiamini serikali katika kufanya biashara hiyo.


0 Comments