TANGAZA NASI

header ads

Dodoma:Wanawake 1000 wajitokeza kumdhamini Rais Magufuli




Na Jackline Kuwanda, DODOMA

Wanawake wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoani Dodoma wamejitokeza kumdhamini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika fomu yake ya kuwania Urais.

Akizungumza na waandishi wa habari Dayana Moses Mwalukwa ambaye ni katibu wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Dodoma mjini amesema wanawake elfu moja (1000) wamejitokeza kumdhamini Rais Magufuli.

Kwa upande wake Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya wilaya ya  Dodoma Mjini (UWT), Joyce George amesema kwa upande wa wakina mama amewasaidia kwa kiasi kikubwa hasa katika upatikanaji wa mikopo huku Joyna Godilisious Makewa  ambaye ni mwanachama wa chama hicho akisema kuwa na ni kada wa UWT akisema amejitokeza kumdhami Rais kwasababu amefanya mambo mengi ikiwemo katika sekta ya Elimu.

June 17 ,2020  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alichukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM kwenye Makao Makuu ya Chama hicho jijini Dodoma ambapo alikabidhiwa fomu hizo na Katibu Mkuu wa Chama hicho Dkt Bashiru Ally.

Post a Comment

0 Comments